BODI YA BONDE LA MTO RUVU KUJENGA ZAIDI YA VISIMA 10 KUNUSURU ADHA YA MAJI.

 


Katika kutekeleza Mpango mkakati wa Majukumu mbalimbali ya Bodi ya Maji Bonde la Mto Ruvu imepanga kujenga zaidi ya Visima 10 katika mikoa ya Morogoro na  Pwani  ili kubakabiliana na changamoto za maji zinazokumba maeneo hayo.


Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu Mhandisi Elibarik Mmasi wakati akitoa taarifa ya Utekelezaji wa Majukumu yanayofanywa na Bodi hiyo na kusema wamekuwa wakitoa vibali kulingana na mahitaji huku wakisimamia vyanzo vya maji kwa maendleo endelevu.


Aidha amesema bodi hiyo imekuwa ikidhiti utoaji maji taka katika viwanda ili kuyaboresha maji hayo yatumike kwa matumizi mengne na kuepukana na uchafunzi wa mazingira sambamba na utunzaji wa vyanzo vya maji .


Pia amebainisha mafanikio yaliyofanywa na bodi hiyo ikiwemo kukarabati na kuboresha miradi sugu ya visima vilivyoanzishwa kwa muda mrefu.


Hata hivyo ameitimisha kwa kutoa rai kwa watu  wanaochimba visima holela na kuwataka wanachi kutoa taarifa ya visima hivyo ili kuepuka madhara yanayojitokeza kutokana na maji yasiyopelekwa maabara kufanyiwa vipimo.



Comments

Popular posts from this blog

HUAWEI AIMS TO USE ITS  “4T”  TECHNOLOGIES TO ENABLE AN ENERGY LANDSCAPE TRANSITION OF 'FROMENERGY CONSUMER TO SUSTAINABLE ENERGY PRODUCER AND ENABLER'

WADAU WA MASUALA YA MAAFA WAJA NA MIKAKATI MADHUBITI YA KUDHIBITI MAAFA

RESHAPING INDUSTRIES WITH AI:HUAWEI CLOUD LAUNCHES PANGU MODELS 3.0 AND ASCEND AI CLOUD SERVICES